.

.

.

.

.

.

.

.
KARIBUNI TUHABARIKE, TUELIMISHANE, TUPEANE HABARI ZA KUKUFANYA UTABASAMU KIDOGO NA MATUKIO YALIYOFANYIWA UCHUNGUZI WA KINA TOKA KILA PEMBE CONTACTS: +255 787 377 722 Email: drweyunga@gmail.com PIA UNAWEZA KUNI FOLLOW KUPITIA INSTAGRAM YANGU @drweyunga | TANGAZA NASI ILI UWAFIKIE WATU WENGI ZAIDI.

Jumapili, 20 Aprili 2014

LIGI KUU UINGEREZA, CHELSEA YASHINDWA KUTAMBA MBELE YA SUNDERLAND

 Timu ya soka ya Sunderland jana iliitibulia Chelsea kukamata usukani wa ligi kuu Uingereza baada ya kuifunga mabao 2-1 katika mchezo ambao mwamuzi Mike Dean alionekana kushindwa kuumudu vyema
 Katika mchezo huo, Chelsea ndio walikuwa wa kwanza kupata bao kupitia kwa Samule Eto'o kunako dakika ya 12, hata hivyo Sunderland ambao niwa mwisho katika msimamo wa ligi pamoja na ushindi wa jana, walisawazisha bao hilo kupitia kwa muuaji wao Wickham kunako dakika ya 18 nala pili kupitia kwa Borin dakika 82 kwa penati. 

Kwa matokeo hayo bado Chelsea wapo nafasi ya pili wakiwa na pointi 75 nyuma ya Liverpool wanaoongoza ligi wakiwa na pointi 77
Kocha msaidizi wa Chelsea Rui Faria akimlalamikia mwamuzi Mike Dean baada ya kutoa penati kwa Sunderland

Hakuna maoni :

Chapisha Maoni