.

.

.

.

.

.

.

.
KARIBUNI TUHABARIKE, TUELIMISHANE, TUPEANE HABARI ZA KUKUFANYA UTABASAMU KIDOGO NA MATUKIO YALIYOFANYIWA UCHUNGUZI WA KINA TOKA KILA PEMBE CONTACTS: +255 787 377 722 Email: drweyunga@gmail.com PIA UNAWEZA KUNI FOLLOW KUPITIA INSTAGRAM YANGU @drweyunga | TANGAZA NASI ILI UWAFIKIE WATU WENGI ZAIDI.

Jumapili, 20 Aprili 2014

LIGI KUU UINGEREZA, LIVERPOOL NJIA NYEUPE YA UBINGWA 2014

 Timu ya soka ya Liverpool imeendelea kujisafishia njia ya kuutwaa ubingwa wa ligi kuu nchini Uingereza msimu huu, baada ya leo kuifunga Norwich mabao 3-0 katika mchezo uliochezwa katika uwanja wa nyumbani wa Norwich, Carrow Road na kushuhudiwa na mashabiki 26,857
 Katika mchezo huo, Liverpool walijipatia bao la kwanza kupitia kwa Sterling kunako dakika ya 4 ya kipindi cha kwanza na kufunga tena bao la tatu dakika ya 64. Luis Suarez aliifungia Liverpool bao la pili dakika ya 11 ya mchezo, na mabao ya Norwich yalifungwa na Hooper dakika ya 53 na Snodgrass dakika ya 77.
Kwa matokeo hayo Liverpool imefikisha pointi 80, tano zaidi ya Chelsea yenye pointi 75 ambayo jana ilikubali kipigo cha mabao 2-1 toka kwa Sunderland. Manchester City wapo nafasi ya tatu na pointi 71. 

Hivi sasa Arsenal wanacheza na Hull City, na hadi dakika ya 16 tunaenda mitamboni timu hizo zilikuwa bado hazijafungana. 

Tutawaletea matokeo baada ya mcheo huo kumalizika

Hakuna maoni :

Chapisha Maoni