Timu ya soka ya Liverpool imeendelea kujisafishia njia ya kuutwaa ubingwa wa ligi kuu nchini Uingereza msimu huu, baada ya leo kuifunga Norwich mabao 3-0 katika mchezo uliochezwa katika uwanja wa nyumbani wa Norwich, Carrow Road na kushuhudiwa na mashabiki 26,857
Katika mchezo huo, Liverpool walijipatia bao la kwanza kupitia kwa Sterling kunako dakika ya 4 ya kipindi cha kwanza na kufunga tena bao la tatu dakika ya 64. Luis Suarez aliifungia Liverpool bao la pili dakika ya 11 ya mchezo, na mabao ya Norwich yalifungwa na Hooper dakika ya 53 na Snodgrass dakika ya 77.
Kwa matokeo hayo Liverpool imefikisha pointi 80, tano zaidi ya Chelsea yenye pointi 75 ambayo jana ilikubali kipigo cha mabao 2-1 toka kwa Sunderland. Manchester City wapo nafasi ya tatu na pointi 71.
Hivi sasa Arsenal wanacheza na Hull City, na hadi dakika ya 16 tunaenda mitamboni timu hizo zilikuwa bado hazijafungana.
Tutawaletea matokeo baada ya mcheo huo kumalizika
Jisajili kwenye:
Chapisha Maoni
(
Atom
)
Hakuna maoni :
Chapisha Maoni