Mchezaji Leighton Baines akiifungia timu yake ya Everton bao la kwanza kwa mkwaju wa penati kunako dakika ya 28 ya mchezo wa ligi kuu nchini Uingereza dhidi ya Manchester United ambayo msimu huu imepoteza kabisa mwelekeo.
Penati hiyo ilipatikana baada ya beki wa Man U, Phil Jones kuunawa mpira
ndani ya 18 wakati akiwa katika harakati za kuondoa hatari langoni mwao.
Katika mchezo huo, Everton walionekana kuelewana sana uwanjani mwanzo hadi mwisho wa mchezo huku wakishangiliwa sana na mashabiki wao.
Mirallas akiifungia Everton bao la pili kunako dakika ya 43 huku mlinda mlango wa Mashetani wekundu David De Gea akijaribu kuucheza mpira huo bila ya mafanikio.
Kwa matokeo hayo katika mchezo huo uliochezwa katika uwanja wa Goodison Park, Everton wamefikisha pointi 69 na kuendelea kubaki nafasi ya tano, huku Man U wakiendelea kubaki nafasi ya saba wakiwa na pointi 57
Duh na leo tena tumepigwa, mwaka huu kila timu inajichukulia pointi kama tumelala!! Wayne Rooney akiwa mnyonge baada ya kupigwa 2-0 na Everton
HIVI NINAYO SHUHUDIA NI KWELI AU NIPO NDOTONI!!! Kocha wa Manchester United David Moyes akiwa haamini kipigo alichokipata
Jisajili kwenye:
Chapisha Maoni
(
Atom
)
Hakuna maoni :
Chapisha Maoni