.

.

.

.

.

.

.

.
KARIBUNI TUHABARIKE, TUELIMISHANE, TUPEANE HABARI ZA KUKUFANYA UTABASAMU KIDOGO NA MATUKIO YALIYOFANYIWA UCHUNGUZI WA KINA TOKA KILA PEMBE CONTACTS: +255 787 377 722 Email: drweyunga@gmail.com PIA UNAWEZA KUNI FOLLOW KUPITIA INSTAGRAM YANGU @drweyunga | TANGAZA NASI ILI UWAFIKIE WATU WENGI ZAIDI.

Jumapili, 20 Aprili 2014

LIGI KUU UINGEREZA, MANCHESTER UNITED YAKUBALI KIPIGO CHA MABAO 2-0 TOKA KWA EVERTON

 Mchezaji Leighton Baines akiifungia timu yake ya Everton bao la kwanza kwa mkwaju wa penati kunako dakika ya 28 ya mchezo wa ligi kuu nchini Uingereza dhidi ya Manchester United ambayo msimu huu imepoteza kabisa mwelekeo. 

Penati hiyo ilipatikana baada ya beki wa Man U, Phil Jones kuunawa mpira 
ndani ya 18 wakati akiwa katika harakati za kuondoa hatari langoni mwao. 

Katika mchezo huo, Everton walionekana kuelewana sana uwanjani mwanzo hadi mwisho wa mchezo huku wakishangiliwa sana na mashabiki wao.
 Mirallas akiifungia Everton bao la pili kunako dakika ya 43 huku mlinda mlango wa Mashetani wekundu David De Gea akijaribu kuucheza mpira huo bila ya mafanikio. 

Kwa matokeo hayo katika mchezo huo uliochezwa katika uwanja wa Goodison Park, Everton wamefikisha pointi 69 na kuendelea kubaki nafasi ya tano, huku Man U wakiendelea kubaki nafasi ya saba wakiwa na pointi 57
 Duh na leo tena tumepigwa, mwaka huu kila timu inajichukulia pointi kama tumelala!! Wayne Rooney akiwa mnyonge baada ya kupigwa 2-0 na Everton
HIVI NINAYO SHUHUDIA NI KWELI AU NIPO NDOTONI!!! Kocha wa Manchester United David Moyes akiwa haamini kipigo alichokipata

Hakuna maoni :

Chapisha Maoni