Mabao matatu yaliyopatikana katika kipindi cha kwanza nacha pili yameiwezesha Arsenal kufikisha pointi 70 na kusimama katika nafasi ya nne katika msimamo wa ligi kuu nchini Uingereza.
Ikicheza ugenini dhidi ya Hull City, Arsenal ilipambana na kupata mabao hayo kupitia kwa Aaron Ramsey dakika ya 31, huku Podolski akitumbukiza kambani mabao mawili, dakika za 45 na 53.
Katika mchezo huo ulioshuhudiwa na mashabiki 24,762 Arsenal walionekana kulisakama lango la Hull City kwa muda mrefu wa mchezo
Mchezaji Podolski akipongezwa na wachezaji wenzake, Olivier Giroud ( aliyemrukia ) na Aaron Ramsey baada ya kufunga goli
Podolski akijipinda na kuachia shuti kali lilikwenda kimiani na kuiandikia Arsenal bao la pili.
Mchezo unaoendelea sasa ni kati ya Manchester United dhidi ya Everton ukiwa katika dakika ya 31, na tayari Everton wanaongoza kwa bao 1-0 lilipatikana kwa njia ya penati dakika ya 28 mfungaji akiwa ni Baines baada ya beki wa Man U Jones kuunawa mpira ndani ya 18 katika harakati za kuokoa mashambulizi langoni mwao.
Everton wanawaendesha puta Man U. Tutawapa matokeo kamili baada ya mchezo huo kumalizika
Jisajili kwenye:
Chapisha Maoni
(
Atom
)
Hakuna maoni :
Chapisha Maoni