.

.

.

.

.

.

.

.
KARIBUNI TUHABARIKE, TUELIMISHANE, TUPEANE HABARI ZA KUKUFANYA UTABASAMU KIDOGO NA MATUKIO YALIYOFANYIWA UCHUNGUZI WA KINA TOKA KILA PEMBE CONTACTS: +255 787 377 722 Email: drweyunga@gmail.com PIA UNAWEZA KUNI FOLLOW KUPITIA INSTAGRAM YANGU @drweyunga | TANGAZA NASI ILI UWAFIKIE WATU WENGI ZAIDI.

Jumapili, 20 Aprili 2014

PAPA AONGOZA MISA YA SIKUKUU YA PASAKA

 Maelfu ya waumini wa dini ya Kikristo waliokusanyika katika viwanja vya kanisa la St.Peters mjini Vatican wakifuatilia misa ya Pasaka iliyokuwa ikiendeshwa na Papa Francis
Kiongozi wa Kanisa Katoliki Duniani, Papa Francis leo ameongoza maelfu ya waumini wa dini ya Kikristo katika misa ya kusherehekea sikukuu ya Pasaka, misa iliyofanyika katika kanisa la St.Peters Vatican. 

Pasaka ni siku ambayo Wakristo wanaadhimisha kufufuka kwa Yesu Kristo. 

Katika misa hiyo, Papa Francis amesisitiza amani, na mazungumzo yenye kufikia muafaka huko Ukraine na Syria, na pia Papa Francis amesisitiza kufikia mwisho kwa mashambulizi yanayofanywa dhidi ya Wakristo nchini Nigeria
Katika misa hiyo, Papa pia katika mahubiri yake amewaombea watu masikini na waliosahaulika katika jamii. Amewataka watu wote duniani kuwa na upendo dhidi ya watu masikini kwa kuwaombea na pia kuwasaidia

Hakuna maoni :

Chapisha Maoni