Kiongozi wa Kanisa Katoliki Duniani, Papa Francis leo ameongoza maelfu ya waumini wa dini ya Kikristo katika misa ya kusherehekea sikukuu ya Pasaka, misa iliyofanyika katika kanisa la St.Peters Vatican.
Pasaka ni siku ambayo Wakristo wanaadhimisha kufufuka kwa Yesu Kristo.
Katika misa hiyo, Papa Francis amesisitiza amani, na mazungumzo yenye kufikia muafaka huko Ukraine na Syria, na pia Papa Francis amesisitiza kufikia mwisho kwa mashambulizi yanayofanywa dhidi ya Wakristo nchini Nigeria
Hakuna maoni :
Chapisha Maoni