Ndugu na jamaa wa waliozama na kivuko huko Korea Kusini wameshikwa na hasira na kulalamikia zoezi la uokoji, wakisema hawaridhishwi na kasi ya uokoaji wa ndugu zao katika kivuko hicho kilichozama jumatano
Polisi waliongezwa kuimarisha ulinzi ili kukabiliana na ndugu hao wenye hasira.Polisi walifanikiwa kuwazuia zaidi ya watu 100 waliotaka kuingia Seoul kutoka kisiwa cha Jindo
Baada ya juhudi za siku tatu, hatimaye wapiga mbizi jana walifanikiwa kuingia ndani ya kivuko hicho na kutoa miili 22 na kufanya idadi ya waliofariki dunia kutokana na kuzama kwa kivuko hicho kufikia 54.
Mpaka sasa watu 174 ndio waliookolewa na wengine 248 bado hawajaonekana
Waokoaji wakibeba moja ya miili ya waliopoteza maisha baada ya kuzama kwa kivuko hicho
Hakuna maoni :
Chapisha Maoni