Waasi nchini Sudan Kusini wameshutumiwa kufanya mauaji makubwa ya zaidi ya watu 200 na wengine 400 wakijeruhiwa kutokana na misingi ya Ukabila. Waasi hao waliuteka mji wa Bentiu na kuwaua raia waliokuwa Kanisani, Msikitini, Hospital na katika kambi ya Umoja wa Mataifa.
Waasi hao walifanikiwa kuuteka mji wa Bentiu baada ya kupambana na majeshi ya serikali wiki iliyopita, na baada ya hapo walianza kutekeleza maasi hayo na wengi wa waliouawa ni watoto na wazee.
Hakuna maoni :
Chapisha Maoni