.

.

.

.

.

.

.

.
KARIBUNI TUHABARIKE, TUELIMISHANE, TUPEANE HABARI ZA KUKUFANYA UTABASAMU KIDOGO NA MATUKIO YALIYOFANYIWA UCHUNGUZI WA KINA TOKA KILA PEMBE CONTACTS: +255 787 377 722 Email: drweyunga@gmail.com PIA UNAWEZA KUNI FOLLOW KUPITIA INSTAGRAM YANGU @drweyunga | TANGAZA NASI ILI UWAFIKIE WATU WENGI ZAIDI.

Jumatano, 23 Aprili 2014

WALIOPOTEZA MAISHA KUFUATIA AJALI YA KIVUKO HUKO KOREA KUSINI WAFIKIA 150, WENGINE 152 BADO HAWAJAONEKANA

 Watu waliofariki dunia baada ya kuzama kwa kivuko huko Korea Kusini jumatano iliyopita sasa wamefikia 150 huku wengine 152 wengi wao wakiwa wanafunzi wa shule iliyopo Ansan nje ya jiji la Seoul wakiwa bado hawajaonekana mpaka sasa.
 Pamoja na juhudi kubwa zilizofanywa na wazamiaji toka kutokea kwa ajali hiyo ya kivuko kilichokuwa kinaelekea katika kisiwa cha kusini cha Jeju, lakini bado kumekuwa na lawama kutoka kwa ndugu waliopoteza maisha wakisema zoezi la uokoji linafanyika kwa kasi ndogo.
Kati ya wahusika 29 wa kivuko hicho, ni 22 tu waliosalimika huku 11 wakikamatwa na kufunguliwa mashitaka kufuatia ajali hiyo.

Hakuna maoni :

Chapisha Maoni