.

.

.

.

.

.

.

.
KARIBUNI TUHABARIKE, TUELIMISHANE, TUPEANE HABARI ZA KUKUFANYA UTABASAMU KIDOGO NA MATUKIO YALIYOFANYIWA UCHUNGUZI WA KINA TOKA KILA PEMBE CONTACTS: +255 787 377 722 Email: drweyunga@gmail.com PIA UNAWEZA KUNI FOLLOW KUPITIA INSTAGRAM YANGU @drweyunga | TANGAZA NASI ILI UWAFIKIE WATU WENGI ZAIDI.

Alhamisi, 31 Julai 2014

EBOLA YASABABISHA SERIKALI YA LIBERIA KUFUNGA SHULE ZOTE

Serikali ya Liberia imetangaza kufunga shule zote nchini humo katika jitihada za kuzuia kusambaa kwa ugonjwa hatari wa Ebola.

Rais Ellen Johnson Sirleaf amesema mbali na uamuzi huo baadhi ya jamii zitalazimika kutotoka katika maeneo wanayoishi.

Vile vile watumishi wasio muhimu wa serikali watatakiwa kutokwenda kazini na kubaki majumbani kwao, huku jeshi la nchi hiyo likisambazwa kuhakikisha maagizo hayo ya serikali yanatekelezwa.

Idadi ya watu waliokufa kwa kuugua Ebola Afrika Magharibi sasa imefikia watu 672, kwa mujibu wa takwimu mpya zilizotolewa na Umoja wa Mataifa.


Hakuna maoni :

Chapisha Maoni