Kocha mpya wa Manchester United
Louis van Gaal amepata ushindi wa kwanza wa kishindo tangu achukue
mikoba ya kuinoa timu hiyo baada ya kuifunga LA Galaxy kwa mbao 7-0
katika mchezo uliohudhuriwa na watazamaji 86,432 huko Rose Bowl,
California.
Katika mchezo huo ambao kiungo wao
mpya Ander Herrera alionyesha kiwango cha juu na kutoa mapande murwa
yaliyochangia ushindi huo ambapo winga Ashley Young, beki Reece
James, walifunga magoli mawili baada ya mshambuliaji Danny Welbeck
kufunga goli la kuongoza katika dakika 13 za mwanzo. Rooney nae
alipachika bao katika mchezo huo.
Ander Herrera akiwajibika
Shinji Kagawa akipiga shuti
Hakuna maoni :
Chapisha Maoni