Kim Kardashian na mumewe Kanye West
wamekuwa hawapati muda wa kuwa pamoja kutokana na kutingwa na
majukumu yao, licha ya kufunga ndoa miezi miwili tu iliyopita.
Kwa mujibu wa taarifa zilizopo
mrembo Kim na rapa Kanye wanaonekana kukerwa na hali hiyo na
wangependa mambo yabadilike na waweze kupata muda mwingi wa kuwa
pamoja.
Wanandoa hao wapya mara ya mwisho
walionekana pamoja nchini Mexico wakiwa katika mapumziko Julai 24,
mwaka huu.
Hakuna maoni :
Chapisha Maoni