Michuano ya Jumuiya ya Madola
imefunguliwa kwa sherehe kubwa zilizofanyika Celtic Park, huko
Glasgow.
Maelfu ya wanamichezo kutoka nchi 71
wameshiriki katika sherehe hizo zilizohudhuriwa na watazamaji 40,000
na kurushwa na vituo vya televisheni kubwa duniani kwa mabilioni ya
watu.
Malkia Elizabeth wa Uingereza alitoa
hotuba na kutangaza rasmi kufunguliwa kwa michuano hiyo, akiwa kwenye
mwenge mkubwa wa Jumuiya ya Madola.
Hakuna maoni :
Chapisha Maoni