.

.

.

.

.

.

.

.
KARIBUNI TUHABARIKE, TUELIMISHANE, TUPEANE HABARI ZA KUKUFANYA UTABASAMU KIDOGO NA MATUKIO YALIYOFANYIWA UCHUNGUZI WA KINA TOKA KILA PEMBE CONTACTS: +255 787 377 722 Email: drweyunga@gmail.com PIA UNAWEZA KUNI FOLLOW KUPITIA INSTAGRAM YANGU @drweyunga | TANGAZA NASI ILI UWAFIKIE WATU WENGI ZAIDI.

Alhamisi, 24 Julai 2014

MIILI 40 KATI YA 298 WALIOPOTEZA MAISHA KATIKA NDEGE YA MALAYSIA YAWASILI UHOLANZI

 Mfalme wa Uholanzi, Willem-Alexander akiwa na Malkia Maxima wakiwa mjini Eindhoven wakisubiri kupokea miili ya abiria waliopoteza maisha yao baada ya ndege ya Malaysia kutunguliwa na waasi wanaoungwa na mkono nchini Ukraine. 

Miili ya abiria 40 kati ya 298 waliopoteza maisha yao katika ndege ya Malaysia iliyotunguliwa na waasi nchini Ukraine, imewasili nchini Uholanzi na kupokelewa na maelfu ya wananchi waliofurika barabarani wakiwa na majonzi kuwapokea wapendwa wao. 

Kati ya abiria hao 298 wakiwemo wahudumu wa ndege hiyo waliopoteza maisha, 193 ni raia wa Uholanzi.
 Msafara wa magari yaliyobeba miili ya abiria 40 kati ya 298 waliofariki dunia katika ajali ya ndege ya Malaysia baada ya kutunguliwa na waasi wanaoungwa mkono na Urusi ukiongozwa na askari waliokuwa katika pikipiki mjini Eindhoven, Uholanzi baada ya kuwasili kutoka Ukraine jana jumatano.

Hakuna maoni :

Chapisha Maoni