.

.

.

.

.

.

.

.
KARIBUNI TUHABARIKE, TUELIMISHANE, TUPEANE HABARI ZA KUKUFANYA UTABASAMU KIDOGO NA MATUKIO YALIYOFANYIWA UCHUNGUZI WA KINA TOKA KILA PEMBE CONTACTS: +255 787 377 722 Email: drweyunga@gmail.com PIA UNAWEZA KUNI FOLLOW KUPITIA INSTAGRAM YANGU @drweyunga | TANGAZA NASI ILI UWAFIKIE WATU WENGI ZAIDI.

Alhamisi, 24 Julai 2014

MWANAMKE ALIYENUSURIKA KUUWAWA SUDAN KWA KUBADILI DINI AWASILI NCHINI ITALIA



Mwanamke wa Sudan aliyenusurika hukumu ya kifo nchini mwake kutokana na kuukana Uislam amesafirishwa kwa ndege hadi Italia baada ya kukaa kwa zaidi ya mwezi mmoja kwenye ubalozi wa Marekani huko Khartoum.



Meriam Yahia Ibrahim Ishag pamoja na familia yake walipokelewa Roma na Waziri Mkuu wa Italia, Matteo Renzi, ambaye alisema leo ni siku ya kusherehekea.



Baba wa Meriam ni muislam mama mkristo na kwa mujibu wa sheria za Kiislam mwanamke huyo alipaswa kuwa muislam na hakutakiwa kubadili dini na kuwa mkristo.
Meriam akutana pia na Papa Francis na kubarikiwa yeye na mtoto wake aliyejifungua akiwa jela.

Hakuna maoni :

Chapisha Maoni