Mwanamke wa Sudan aliyenusurika
hukumu ya kifo nchini mwake kutokana na kuukana Uislam amesafirishwa
kwa ndege hadi Italia baada ya kukaa kwa zaidi ya mwezi mmoja kwenye
ubalozi wa Marekani huko Khartoum.
Meriam Yahia Ibrahim Ishag pamoja na
familia yake walipokelewa Roma na Waziri Mkuu wa Italia, Matteo
Renzi, ambaye alisema leo ni siku ya kusherehekea.
Baba wa Meriam ni muislam mama
mkristo na kwa mujibu wa sheria za Kiislam mwanamke huyo alipaswa
kuwa muislam na hakutakiwa kubadili dini na kuwa mkristo.
Meriam akutana pia na Papa Francis na kubarikiwa yeye na mtoto wake aliyejifungua akiwa jela.
Meriam akutana pia na Papa Francis na kubarikiwa yeye na mtoto wake aliyejifungua akiwa jela.
Hakuna maoni :
Chapisha Maoni