Jeshi la Maji la Kenya limerejeshwa
tena kusaidi operesheni ya jeshi la polisi eneo la Likoni, Mombasa
baada ya kuibuka hofu juu ya ripoti za kuonekana watu wenye silaha
wakiranda eneo hilo.
Kutokana na taarifa hizo za hofu ya
kushambuliwa wazazi walilazimika kuwaondoa shuleni watoto wao jana
huku wafanyabiashara nao wakifunga biashara zao katika eneo hilo la
Likoni, ambapo baadae vyombo vya dola vilibaini bomu la kutupwa kwa
mkopo katika kitongoji cha Soweto.
Hakuna maoni :
Chapisha Maoni