.

.

.

.

.

.

.

.
KARIBUNI TUHABARIKE, TUELIMISHANE, TUPEANE HABARI ZA KUKUFANYA UTABASAMU KIDOGO NA MATUKIO YALIYOFANYIWA UCHUNGUZI WA KINA TOKA KILA PEMBE CONTACTS: +255 787 377 722 Email: drweyunga@gmail.com PIA UNAWEZA KUNI FOLLOW KUPITIA INSTAGRAM YANGU @drweyunga | TANGAZA NASI ILI UWAFIKIE WATU WENGI ZAIDI.

Jumatano, 20 Agosti 2014

AJALI YA KUTISHA YATOKEA TABORA, WATU 16 WAFARIKI DUNIA NA WENGINE 75 WAJERUHIWA

Watu zaidi ya 16 wamefariki dunia na wengine zaidi ya 75 wmejeruhiwa baada ya mabasi mawili waliyokuwa wakisafiria kugongana katika kijiji cha Mlogolo wilayani Sikonge mkoani Tabora jana.

Ajali hiyo imetokea jana baada ya Basi la Kampuni ya Sabena lenye namba za usajiri T 110 ARV linalofanya safari zake  Mbeya - Tabora kugongana uso kwa uso na basi la AM Dreamline lenye namba za usajiri T 803 ATN lililokuwa likitokea Mwanza kwenda Mpanda.

Kamanda wa polisi mkoa wa Tabora, ACP Suzan Kaganda amesema kuwa ajali hiyo imetokea maeneo ya Mlogolo takribani kilometa 3 kutoka wilayani Sikonge. 

Kamanda Kaganda amethibitisha idadi ya watu hao waliofariki pamoja na majeruhi baada ya kutembelea eneo la ajali na kufika katika chumba cha kuhifadhia maiti.

Hakuna maoni :

Chapisha Maoni