Kundi linalotaka kuunda Taifa la
Kiislam nchini Irak la (IS), limetoa video inayoonyesha kitendo cha
kuuwawa kwa kukatwa kichwa mwandishi wa habari Marekani, James Foley,
aliyekamatwa nchini Syria mwaka 2012.
Wapiganaji wa kundi hilo wamesema wamemuua mwandishi huyo ili kulipa kisasi kitendo cha Mareakani kufanya mashambulizi ya anga yanayofanywa dhidi ya wapiganaji wa kundi hilo nchini Irak.
Mama wa Foley, Diane amesema kupitia
Facebook kuwa anajivunia mtoto wake huyo, kutokana na ujasiri wake wa
kujitolea maisha yake ili kutoa habari za mateso waliyokuwa wakipata
wananchi wa Syria.
Hakuna maoni :
Chapisha Maoni