.

.

.

.

.

.

.

.
KARIBUNI TUHABARIKE, TUELIMISHANE, TUPEANE HABARI ZA KUKUFANYA UTABASAMU KIDOGO NA MATUKIO YALIYOFANYIWA UCHUNGUZI WA KINA TOKA KILA PEMBE CONTACTS: +255 787 377 722 Email: drweyunga@gmail.com PIA UNAWEZA KUNI FOLLOW KUPITIA INSTAGRAM YANGU @drweyunga | TANGAZA NASI ILI UWAFIKIE WATU WENGI ZAIDI.

Jumatano, 20 Agosti 2014

MHE. BALOZI BATILDA S. BURIAN AKUTANA NA KUFANYA MAZUNGUMZO NA MKURUGENZI MKUU MPYA WA TAASISI YA “SHELTER AFRIQUE”, NAIROBI

Kutoka kulia ni Mhe. Balozi Dr. Batilda S. Burian akifanya mazungumzo ofisini kwake na Mkurugenzi Mkuu Mpya wa taasisi ya Shelter Afrique Bw. James Mugerwa(Katikati) ambaye aliambatana na afisa wake Bw. Vipya Harawa (Kushoto) ambaye ni Mkurugenzi wa masuala ya ushirikiano katika taasisi hiyo.
**************************
Bw. James Mugerwa, Mkurugenzi Mkuu Mpya wa Taasisi ya Shelter Afrique yenye makao yake makuu hapa jijini Nairobi amemtembelea Mhe. Balozi Batilda ofisini kwake kwa ajili ya kujitambulisha kutokana na kuchaguliwa kwake hivi karibuni kuwa Mkurugenzi Mpya wa Taasisi hii muhimu ambayo imekuwa ikijishughulisha na utoaji wa mikopo nafuu kwa nchi wanachama wake kwa ajili uendelezaji wa miji na makazi bora nafuu, ambapo Tanzania ni moja ya nchi mwanachama katika taasisi hii.

Mhe. Batilda ni Balozi wa Tanzania nchini Kenya ambaye pia ni Mwakilishi wa Kudumu wa Tanzania kwenye Mashirika ya Umoja wa Mataifa ya UN-Habitat na UNEP yenye makao yake makuu hapa Nairobi.

Katika mazungumzo, Bw. Mugerwa alitoa shukrani za pekee kwa Tanzania kwa jinsi ambavyo imekuwa ikitoa ushirikiano mkubwa kwa Taasisi hii na kuahidi kudumisha na kuendeleza ushirikiano ambao umekuwepo.

Hakuna maoni :

Chapisha Maoni