.

.

.

.

.

.

.

.
KARIBUNI TUHABARIKE, TUELIMISHANE, TUPEANE HABARI ZA KUKUFANYA UTABASAMU KIDOGO NA MATUKIO YALIYOFANYIWA UCHUNGUZI WA KINA TOKA KILA PEMBE CONTACTS: +255 787 377 722 Email: drweyunga@gmail.com PIA UNAWEZA KUNI FOLLOW KUPITIA INSTAGRAM YANGU @drweyunga | TANGAZA NASI ILI UWAFIKIE WATU WENGI ZAIDI.

Jumatano, 20 Agosti 2014

RAIS ELLEN JOHNSON SIRLEAF APIGA MARUFUKU KUTEMBEA USIKU JIJINI MONROVIA

Nchi ya Liberia imepiga marufuku watu kutembea usiku na kuzuia watu kutoka katika eneo moja la Jiji la Monrovia katika jitihada za kukabiliana na mlipuko wa Ebola.

Rais Ellen Johnson Sirleaf amesema amri hiyo ya kutotembea usiku inaanzia saa tatu usiku hadi saa kumi na mbili alfajiri.

Amesema kuwa kila nyendo za watu katika muda huo zitazuiliwa ambapo pia watu wa eneo la Magharibi mwa Mji wa Monrovia hawaturuhusiwa kutoka nje ya eneo hilo.

Wakati huo huo madaktari watatu wanaougua Ebola walioanza kutibiwa kwa kutumia dawa zilizo kwenye majaribio wameonyesha dalili za kupata ahueni, Waziri wa Habari wa Lewis Brown amesema.
           Popo huyu mla matunda ndio anayesadikika kusambaza virusi vya Ebola

Hakuna maoni :

Chapisha Maoni