Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Balozi Seif Ali Iddi kati
kati akiwa katika picha ya pamoja na uongozi wa Jumuiya ya Watanzania
wanaosoma Nchini Korea ya Kusini { KOIKA } uliofika nyumbani kwake
kujitambulisha rasmi baada ya kushika wadhifa huo.Kushoito ya Balozi
Seif ni Rais wa Jumuiya hiyo ya KOIKA Nd. Steven Katemba na Makamu wa
Rais wake Nd. Bukheit Juma. (Picha na Hassan Issa wa – OMPR –
ZNZ).
PRESS RELEASE
Jumuiya ya
Wanafunzi wa Kitanzania wanaosoma Nchini Korea ya Kusini {KOIKA}
imejipanga kuwa kiunganishi kizuri cha wanataaluma wa Korea ya Kusini
na wale wa Kitanzania kwa lengo la kudumisha uhusiano uliopo kati ya
nchi mbili hizo.
Rais wa KOIKA
aliyekuwa kinara wa Ujumbe wa Viongozi Wanne wa Jumuiya hiyo Ndugu
Steven Katemba alieleza hayo wakati wa mazungumzo yake na Makamu wa
Pili wa Rais wa Zanzibar Balozi Seif Ali Iddi Nyumbani kwake Mazizini
Nje kidogo ya Mji wa Zanzibar.
Nd. Steven na
ujumbe wake ambao wapo Nchini Tanzania kujitambulisha rasmi baada ya
kuchaguliwa kwao kushika dhamana hiyo ya Uongozi wa Jumuiya mnamo
Mwezi Mei mwaka huu alisema zipo fursa nyingi za kimasomo na uhusiano
Nchini Korea Kusini ambazo Vijana wa Kitanzania wanaweza
kuzichangamkia.
Alieleza kwamba
Korea ya Kusini iliyopo Bara la Asia ni miongoni mwa Nchi chache za
Bara hilo ziliyopiga hatua kubwa za maendeleo na kiuchumi kiasi
kwamba Tanzania inaweza kujifunza kupitia maendeleo hayo.
Alisema Jumuiya
yao mbali ya kuanzishwa kwa lengo la kusaidiana kupambana na matatizo
yanayowakabili katika mafunzo yao lakini pia imejipanga kushiriki
katika shughuli za Kijamii hapa Tanzania.
Rais huyo wa
Jumuiya ya Wanafunzi wa Kitanzania wanaosoma Nchini Korea ya Kusini
alifahamisha kwamba wanachama wa jumuiya hiyo tayari wameshajipanga
kufanya kazi za Kijamii hivi karfibuni katika Nyumba za Wazee ziliopo
Mtaa wa Sebleni Mjini Zanzibar.
Alisema kazi
hizo zitakuwa ni pamoja na kufanya usafi utakaoambatana na
kubadilishana mawazo na wazee hao ambao tayari wameshatumia muda wao
mwingi wa maisha katika Kujenga Taifa la Tanzania.
Akitoa Shukrani
zake Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Balozi Seif Ali Iddi
aliipongeza Jumuiya hiyo ya Wanafunzi wa Kitanzania wanaosoma Nchini
Korea Kusini kwa uamuzi wao wa kuunda Jumuiya itakayowasaidia
kukabiliana na changa moto zozote zitakazojitokeza mbele yao.
Balozi Seif
alisema kitendo cha vijana hao kuamua kujishirikisha katika shughuli
za Kijamii kinaweza kuamsha ari na chachu kwa vijana wengine nchini
na hata wale wanaosoma mataifa wengine kuunda vikundi kama hivyo.
Makamu wa Pili
wa Rais wa Zanzibar Balozi Seif aliueleza Uongozi wa Jumuiya hiyo ya
Koika kwamba uhusiano uliopo kati ya Korea ya Kusini na Jamuhuri ya
Muungano wa Tanzania ni mkubwa na Vijana hao wana haki na wajibu wa
kusaidia kuudumisha uhusiano huo muhimu kwa ustawi wa pande zote
mbili.
Zaidi ya
Wanafunzi mia Tisa na Kumi wa Kitanzania wanasoma Nchini Korea ya
Kusini ambao kati ya hao Mia Moja na Mbili wanatoka Visiwani
Zanzibar.
Othman Khamis
Ame
Ofisi ya Makamu
wa Pili wa Rais wa Zanzibar
20/8/2014.
Hakuna maoni :
Chapisha Maoni