Polisi nchini Kenya jana usiku
wamewapiga risasi na kuwauwa watuhumiwa watatu wa ujambazi na
kukamata silaha aina ya AK-47 katika eneo la Mbaruk katika barabara
ya Nairobi-Nakuru.
OCPD Bernad Kioko amesema genge hilo
lilikuwa linafuatilia lori lililokuwa limebeba vifaa vya umeme wakati
waliponaswa na polisi baada ya kupatiwa taarifa zao.
Genge hilo la majambazi inasemekana
limekuwa likifanya uhalifu katika maeneo ya Nakuru na Nyahururu kwa
muda kabla ya kunaswa jana majira ya saa tatu usiku.
Hakuna maoni :
Chapisha Maoni