Rais Jacob Zuma amesema raia 67 wa
Afrika Kusini wamekufa katika tukio la kuanguka kwa jengo la kulala
wageni la Muhubiri wa Nigeria, TB Joshua huko Lagos wiki iliyopita.
Rais Zuma amesema tukio hilo ni
janga kubwa kuwahi kuwakuta raia wa Afrika Kusini wakiwa nje ya nchi
katika historia ya nchi hiyo.
Vikosi vya uokoaji vya Nigeria
vimesema karibu miili 70 ya watu imetolewa kwenye vifusi vya jengo
hilo la ghorofa mbili.
Hakuna maoni :
Chapisha Maoni