Wakazi wa mji wa Bukoba mkoani Kagera wapo mbioni kuondokana na adha ya kukosa ukumbi wa kisasa kwa ajili ya shuhghuli mbalimbali baada ya ukumbi wa Anjelina kuwa mbioni kukamilika.
Ukumbi huo wa kisasa uliopo Rwamishenyi nje kidogo ya mji wa Bukoba, utakuwa ni maalumu kwa ajili ya shughuli za Send Off, Harusi, mikutano ya aina mbalimbali, mahafali n.k.
Ukumbi huo ambao utakuwa umesheheni vifaa vyote vya kisasa ndani ikiwa ni pamoja na viyoyozi kote, unatarajiwa kuanza kutoa huduma kuanzia mwezi wa kumi na mbili mwaka huu ( Desemba 2014 ).
Ukumbi wa Anjelina ukiwa katika hatua za mwisho kukamilisha ujenzi wake.
Muonekano wa ukumbi huo ambao pia una garden kubwa naya kuvutia
Hakuna maoni :
Chapisha Maoni