Wanakijiji wapatao 200 nchini India
wamenyoa vipara katika kuomboleza kifo cha nyani wa hekalu lao.
Nyani huyo wa hekalu alianguka
kwenye bwawa na kufa maji baada ya kufukuzwa na mbwa.
Kwa kuhofia kifo cha nyani huyo
kitasababisha bahati mbaya kwao, wanakijiji waliandaa mazishi ya
nyani huyo kwa kumchoma moto kwa taratibu za mazishi ya Kihindu.
Pia wanavijiji wengine 700 wao nao
walinyoa ndevu zao, katika kuomboleza kifo cha nyani huyo ambapo kwa
kawaida mnyama huyo huchukuliwa kama Mungu kwa waumini wa thehebu la
Kihindu.
Hakuna maoni :
Chapisha Maoni