Watu wapatao 50 wameuwawa katika
mashambulizi ya ndege ya anga yaliyofanywa na serikali ya Syria,
katika mji unaoshikiliwa na upinzani.
Shirika la Syria la Kuratibu Haki za
Binadamu limesema miongoni mwa waliokufa ni watoto sita katika mkoa
wa Homs, kufuatia mkoa huo kudondoshewa mabomu kwa siku mbili.
Makumi ya wapiganaji wanaoshikilia
mji huo wamekufa, shirika hilo la Uingereza limesema. Taarifa zaidi
zinasema watoto wengine 34 wamekufa katika eneo lingine
linaloshikiliwa na waasi baada kupatiwa chanjo iliyoharibika.
Hakuna maoni :
Chapisha Maoni