.

.

.

.

.

.

.

.
KARIBUNI TUHABARIKE, TUELIMISHANE, TUPEANE HABARI ZA KUKUFANYA UTABASAMU KIDOGO NA MATUKIO YALIYOFANYIWA UCHUNGUZI WA KINA TOKA KILA PEMBE CONTACTS: +255 787 377 722 Email: drweyunga@gmail.com PIA UNAWEZA KUNI FOLLOW KUPITIA INSTAGRAM YANGU @drweyunga | TANGAZA NASI ILI UWAFIKIE WATU WENGI ZAIDI.

Alhamisi, 23 Oktoba 2014

CANADA YASEMA HAITATISHWA NA VITISHO VYA MAGAIDI

Waziri Mkuu wa Canada Stephen Harper amesema nchi yake kamwe haitatishwa baada ya kutokea shambulio kubwa katika bunge lake la taifa katika Jiji la Ottawa.

Bw. Harper amesema tukio hilo linasisitiza Canada kuongeza maradufu jitihada zake za kupambana na makundi ya ugaidi.

Mapema mtu mwenye silaha alimuua mwanajeshi katika eneo la kumbukumbu ya vita la Ottawa, kabla ya kuuwawa katika mapambano ya risasi na polisi ndani ya bunge.

Tukio hilo limetokea saa chache baada ya Canada kuongeza kiwango cha hatari ya tishio la ugaidi.

Siku ya jumatatu mwanajeshi mmoja aliuwawa kwa kugongwa na gari na kisha dereva wake kukimbia huko Quebec, ambapo muhsika ni muislam aliyeslimu.
                  Picha ya mtuhumiwa aliyeuwawa baada ya kumuua mwanajeshi

Hakuna maoni :

Chapisha Maoni