Ikicheza ugenini, washika bunduki wa jiji la London Arsenal wameibuka na ushindi wa mabao 2-1 dhidi ya wenyeji wao Anderlecht katika mchezo wa ligi ya mabingwa Barani Ulaya, mchezo uliochezwa usiku wa kuamkia leo.
Wakionekana kuukamia mchezo huo ili kuibuka na ushindi, vijana hao wanaonolewa na Mfaransa Arsene Wenger iliwabidi wafanye kazi ya ziada kuepuka aibu ugenini baada ya kujipatia mabao yao dakika za majeruhi.
Mabao mawili ya dakika za lala salama yaliwekwa kimiani na Kieran Gibbs katika dakika ya 89 na dakika ya 90 Lukas Podolski akafunga bao la pili.
Wenyeji Anderlecht ndio waliokuwa wa kwanza kupata bao lililowekwa kimiani na Andy Najar katika dakika ya 70 ya mchezo huo.
Jisajili kwenye:
Chapisha Maoni
(
Atom
)
Hakuna maoni :
Chapisha Maoni