Rwanda imeimarisha ufuatiliaji wa
wageni wanaoingia nchini humo ili kudhibiti Ebola, kwa kuwaagiza
wageni kutoka nchi za Marekani na Hispania kutuma kila siku ujumbe wa
hali za afya zao pindi waingiapo Rwanda.
Waziri wa Afya wa Rwanda Bi. Agnes
Binagwaho amesema wageni wote wanaotokea nchi hizo wanapaswa kutuma
ujumbe huo tangu siku ya kwanza wawapo Rwanda kwa siku 21, hususan
wale waliokuwa Marekani na Hispania katika wiki tatu zilizopita.
Hakuna maoni :
Chapisha Maoni