.

.

.

.

.

.

.

.
KARIBUNI TUHABARIKE, TUELIMISHANE, TUPEANE HABARI ZA KUKUFANYA UTABASAMU KIDOGO NA MATUKIO YALIYOFANYIWA UCHUNGUZI WA KINA TOKA KILA PEMBE CONTACTS: +255 787 377 722 Email: drweyunga@gmail.com PIA UNAWEZA KUNI FOLLOW KUPITIA INSTAGRAM YANGU @drweyunga | TANGAZA NASI ILI UWAFIKIE WATU WENGI ZAIDI.

Ijumaa, 31 Oktoba 2014

MELI YA UINGEREZA YAWASILI SIERRA LEONE KUSAIDIA KUKABILIANA NA EBOLA

Meli ya Uingereza imewasili Sierra Leone kusaidia kukabiliana na mlipuko wa ugonjwa wa Ebola, katika nchi za Afrika Magharibi.

Meli hiyo ya Royal Fleet Auxiliary Argus imebeba shehena ya vyakula, vifaa tiba, pamoja na magari 32 ya aina ya pick-up, katika kusaidia kukabiliana zaidi na virusi vya Ebola.

Madaktari, wauguzi pamoja na wanajeshi wa Uingereza wapo kwenye meli hiyo, iliyotia nanga katika Jiji la Freetown.

Ugonjwa wa Ebola umeshauwa karibu watu 5,000 waliopata maambukizi yake ambao zaidi ya watu 10,000 wakiwa katika nchi za Afrika ya Magharibi.

Hakuna maoni :

Chapisha Maoni