Ndege za kijeshi za Marekani
zimedondosha silaha, vifaa vya kijeshi pamoja na vifaa tiba kwa
wapiganaji wa Kikurdi wanaopambana na kundi la Dola ya Kiislam (IS)
katika mji wa Syria wa Kobane.
Makao Makuu ya Jeshi la Marekani
imesema ndege aina ya C-130 zimefanya safari za kudondosha vitu hivyo
kwa mamlaka ya wakurdi nchini Irak.
Mashambulizi ya anga ya Marekani
yamesaidia kuwarejesha nyuma wapiganaji wa IS, katika mji wa Kobane
uliopo karibu na mpaka wa Uturuki.
Hakuna maoni :
Chapisha Maoni