Spika wa Bunge la Uganda Rebecca
Kadaga amewapongeza wabunge wasio na hofu na waongeaji katika bunge
la tisa kwa kupigania maslahi ya wananchi, ambapo amsema viongozi wa
aina hiyo wanachangia kuishinikiza serikali kuboresha utoaji huduma
bora kwa wananchi.
Mbali na pongezi hiyo kwa wabunge
wakosoaji serikali Spika Kadaga amewataka wananchi kuwachagua wabunge
shupavu na majasiri ambao wanaweza kumudu presha na kupigania maslahi
ya wananchi.
Spika Kadaga amekuwa muhimili mkuu
katika kuchangia kutoa uhuru kwa wabunge wa Uganda kuisimamia
serikali, licha ya kutokea chama tawala cha NRM kiasi wakati mwingine
amejikuta akiwa kwenye misuguano na serikali.
Hakuna maoni :
Chapisha Maoni