Watu wapatao nane wamekufa kwa
mlipuko uliotokea kwenye moja ya vituo vikuu vya jimbo la Gombe
kaskazini-mashariki mwa Nigeria.
Vyanzo kutoka mji wa Gombe, vimesema
watu wengi wamejeruhiwa katika mlipuko huo katika muda wenye
pirikapirika nyingi.
Mashahidi wameliambia shirika la AFP
kuwa milipuko ilitokea kwenye mifuko mitatu iliyojaa milipuko.
Gombe inapakana na majimbo matatu
yaliyo kwenye hali ya tahadhari kutokana na harakati za wapiganaji wa
kundi la Boko Haram.
Hakuna maoni :
Chapisha Maoni