.

.

.

.

.

.

.

.
KARIBUNI TUHABARIKE, TUELIMISHANE, TUPEANE HABARI ZA KUKUFANYA UTABASAMU KIDOGO NA MATUKIO YALIYOFANYIWA UCHUNGUZI WA KINA TOKA KILA PEMBE CONTACTS: +255 787 377 722 Email: drweyunga@gmail.com PIA UNAWEZA KUNI FOLLOW KUPITIA INSTAGRAM YANGU @drweyunga | TANGAZA NASI ILI UWAFIKIE WATU WENGI ZAIDI.

Ijumaa, 31 Oktoba 2014

WAZAZI WATAKAOHAKIKISHA WATOTO WA KIKE WANASOMA SHULE KUPEWA NG'OMBE NCHINI KENYA

Ng'ombe watakuwa wanagaiwa kwa wakinababa kaskazini mwa Kenya, ambao watahakikisha watoto wao wakike wanaendelea na masomo.

Gavana wa kaunti ya Laikipia Joshua Irungu, amesema ngombe tisa watagaiwa kwa wakinababa watakaotimiza suala hilo katika maeneo yawafugaji vijijini.

Kwa mujibu wa sheria za Kenya, mzazi atakayeshindwa kumpeleka mtoto wake shule anaweza kupatiwa adhabu ya kifungo jela.

Hata hivyo ndoa za utotoni ni jambo ambalo limezoeleka mno katika jamii za wafugaji, ambazo hutegemea zaidi kupata mahari ya ng'ombe.

Hakuna maoni :

Chapisha Maoni