.

.

.

.

.

.

.

.
KARIBUNI TUHABARIKE, TUELIMISHANE, TUPEANE HABARI ZA KUKUFANYA UTABASAMU KIDOGO NA MATUKIO YALIYOFANYIWA UCHUNGUZI WA KINA TOKA KILA PEMBE CONTACTS: +255 787 377 722 Email: drweyunga@gmail.com PIA UNAWEZA KUNI FOLLOW KUPITIA INSTAGRAM YANGU @drweyunga | TANGAZA NASI ILI UWAFIKIE WATU WENGI ZAIDI.

Jumamosi, 29 Novemba 2014

BUNGE LAHAIRISHWA TENA HADI SAA KUMI JIONI

Bunge limehairishwa kwa mara ya pili leo, sasa litakaa saa kumi jioni ili kutoa muda kwa kamati kuendelea kusaka maridhiano, ili Bunge litakapokaa jioni muafaka uweze kufikiwa bila kuwepo na mivutano. 

Mh Spika Anne Makinda amefikia uamuzi huo baada ya kuombwa bunge kuahirishwa kwa saa moja na Waziri wa Nchi, Mh William Lukuvi ili wabunge wa CCM waweze kukutana na kuafikiana ili bunge likapokaa tena waweze kuwa wamoja kwa mustakabali wa nchi yetu. 

Hata hivyo Mh Zitto Kabwe yeye aliomba masaa mawili, Mh Mbatia akaomba wapewe muda zaidi, na katika kuhitimisha, Mh Spika akasema bunge litakutana saa kumi jioni.

Hakuna maoni :

Chapisha Maoni