Korea Kaskazini imetishia kufanya
majaribio ya silaha za nyuklia, katika kujibu mapigo hatua ya Umoja
wa Mataifa kuichunguza nchi hiyo kuhusiana na ukiukaji wa haki za
binadamu.
Wizara yake ya mambo ya nje hii leo
imeishutumu Marekani kwa kuchochea wito wa hivi karibuni wa Umoja wa
Mataifa kuichunguza Korea Kaskazini.
Korea Kaskazini katika miaka ya
nyuma ilifanya majaribio ya nyuklia katika mwaka 2006, 2009 na 2013.
Tishio hilo limekuja baada ya picha
za setelaiti kuonyesha kuwepo kwa shughuli zinazoendelea kwenye eneo
la mitambo ya nyuklia ya Korea Kaskazini.
Hakuna maoni :
Chapisha Maoni