.

.

.

.

.

.

.

.
KARIBUNI TUHABARIKE, TUELIMISHANE, TUPEANE HABARI ZA KUKUFANYA UTABASAMU KIDOGO NA MATUKIO YALIYOFANYIWA UCHUNGUZI WA KINA TOKA KILA PEMBE CONTACTS: +255 787 377 722 Email: drweyunga@gmail.com PIA UNAWEZA KUNI FOLLOW KUPITIA INSTAGRAM YANGU @drweyunga | TANGAZA NASI ILI UWAFIKIE WATU WENGI ZAIDI.

Alhamisi, 20 Novemba 2014

MAHAKAMA YA RUFAA YAKAZIA AMRI YA KUKAMATWA KIONGOZI WA WIKILEAKS

Mahakama ya rufaa ya nchini Sweden imekazia hukumu ya hati ya kukamatwa muasisi wa Wikileaks, Julian Assange, na kuhojiwa kwa kesi ya udhalilishaji wa kingono.

Mahakama hiyo ya rufaa imekataa ombi la rufaa ya Assange, ya kutengua amri ya kukamatwa kwake iliyotolewa mnamo mwaka 2010.

Assange, ambaye amekanusha tuhuma hizo amepatiwa hifadhi katika ubalozi wa Ecuador Jijini London nchini Uingereza.

Mbali na kuhitajika Sweden kwa kesi hiyo, Assange anahitajika nchini Marekani kwa kosa la kuvujisha siri za nchi hiyo.

Hakuna maoni :

Chapisha Maoni