Mama Sarah Obama, ambaye ni bibi wa
rais wa Marekani ameiliambia gazeti moja la nchi hiyo kuwa anatarajia
kumualika rais Barack Obama kutembelea Kenya.
Mama Sarah anatarajia kukutana na
rais Obama hivi karibuni kwenye Ikulu ya Marekani Jijini Washington
DC, ambapo atatumia fursa hiyo kumuomba mjukuu wake kuitembelea
Kenya.
Rais Obama aliahidi kuja katika nchi
ya Kenya aliyozaliwa baba yake, kabla ya kumalizika kwa muda wake wa
urais Januari 2017.
Hakuna maoni :
Chapisha Maoni