Mchezaji mkongwe maarufu nchini
Brazil, Pele amesema anaendelea vizuri baada ya kuhamishiwa kitengo
cha uangalizi maalum, akitibiwa maambukizi ya njia ya haja ndogo.
Hospitali ya Albert Einstein iliyopo
Sao Paulo Pele (74) ambaye alitwaa kombe la dunia mara tatu
amehamishiwa kitengo hicho baada ya hali yake kutoimarika kitabibu.
Taarifa zinadai kuwa Pele, ambaye
alilazwa hospitali siku ya jumatatu, amehamishiwa kwenye chumba cha
wagonjwa mahututi.
Hakuna maoni :
Chapisha Maoni