Polisi nchini Uganda wameomba
ushauri wa wataalamu wa picha kubaini iwapo picha za utupu za
mwanamuziki Desire Lusinda zilizosambazwa mitandaoni ni zake halisi
ama zimefanyiwa ujanja.
Hatua hiyo ya polisi ni sehemu ya
uchunguzi mpana wa tukio hilo, lililozua mjadala mkubwa nchini
Uganda, na kuvuka mipaka ya nchi hiyo kutokana na umaarufu Desire
Luzinda.
Tangu kusambazwa kwa picha hizo
kumekuwa na makundi mawili moja linamlaumu msanii Desire kwa mienendo
michafu, huku wengine wakimtetea na kusema msanii huyo ni mhanga wa
tukio hilo.
Hakuna maoni :
Chapisha Maoni