Rais wa Ufaransa Francois Hollande
atawasili nchini Guinea, na kuwa kiongozi wa kwanza kutoka mataifa ya
magharibi kutembelea nchi inayokabiliwa na ugonjwa hatari wa Ebola.
Rais Hollande atatoa ujumbe wa
mshikamano na Guinea, ambapo watu zaidi ya 1,200 wamefariki dunia kwa
Ebola.
Ufaransa imeahidi dola milioni 125,
kusaidia kukabiliana na ugonjwa huo kwa kuchangia ufunguaji wa vituo
kadhaa vya afya nchini Guinea.
Hakuna maoni :
Chapisha Maoni