Karibu watu milioni 5 wanaoishi
kinyume na sheria nchini Marekani wanaweza kunusurika kurejeshwa nchi
walizotoka, kwa mujibu wa mabadiliko ya mfumo wa uhamiaji.
Katika hotuba yake Rais Barack Obama
amewataka watunga sheria, kutoka katika kiza na kuja na sheria zilizo
sawa za uhamiaji.
Hata hivyo chama cha Republican
kimesema vitendo bila kuwa na uwezo katika Baraza la Congress, ni
zaidi ya mamlaka na kusema kuwa uhusiano baina ya mihimili hiyo
miwili utatibuka.
Marekani inawahamiaji haramu milioni
11, na kwa mwaka huu watoto ambao wanaingia katika mipaka ya nchi
hiyo wameibua mgogoro.
Wahamiaji haramu Marekani wakifuatilia hotuba ya rais Barack Obama
Hakuna maoni :
Chapisha Maoni