Dereva aliyekuwa akitamka kwa
kiarabu maneno yanayomaanisha 'Mungu ni Mkubwa', amewagonga watembea
kwa miguu katika eneo la Dijon nchini Ufaransa na kuwajeruhi watu 11,
wawili kati yao wapo mahututi.
Mtu huyo alikamatwa baada ya
kuwalenga kuwagonga watu katika maeneo matano tofauti ya mji huo,
katika muda usiozidi tafuati ya nusu saa.
Inasemekana mtu huyo akili zake
hazikuwa zimetulia, na alikuwa akitibiwa kwenye hospitali za wagonjwa
wa akili.
Polisi wa Ufaransa siku ya jumamosi
walimpiga risasi na kufa mwanaume mmoja aliyekuwa akitaka
kuwashambulia kwa kisu huku akitamka kwa sauti 'Mungu ni Mkubwa'.
Hakuna maoni :
Chapisha Maoni