Mgombea urais wa Tunisia, Beji Caid
Essebsi amedai kupata ushindi katika uchaguzi wa kwanza huru wa
urais, huku matokeo yakionyesha kupata asilimia 55 ya kura zote.
Wafuasi wa Essebsi mwenye umri wa
miaka 88, wamekuwa wakisherehekea ushindi wake katika mji mkuu Tunis.
Wapiga kampeni wa kambi ya mpinzani
wake, ambaye alikua akikaimu urais Moncef Marzouki, wamesema matokeo
yanakaribiana mno kuweza kutangaza mshindi.
Hakuna maoni :
Chapisha Maoni