Polisi nchini Pakistan wamesema
wemewakamata watu kadhaa wanaotuhumiwa kuhusika na tukio la mauaji
yaliyofanyika kwenye shule inayoendeshwa na jeshi huko Peshawar wiki
iliyopita.
Waziri wa Mambo ya Ndani wa Pakistan
amesema watu hao ambao wote ni wanaume, walihusika kusaidia kuwezesha
shambulio hilo lililouwa watu 141, wakiwemo watoto 132.
Waziri huyo Chaudhry Nisar Ali Khan
ameongeza kuwa taarifa za kiitelijensia zinaonyesha kuwa shambulio
lingine linapangwa kufanyika. Wapiganaji wa Taliban wamekiri kuhusika
na tukio hilo.
Hakuna maoni :
Chapisha Maoni