.

.

.

.

.

.

.

.
KARIBUNI TUHABARIKE, TUELIMISHANE, TUPEANE HABARI ZA KUKUFANYA UTABASAMU KIDOGO NA MATUKIO YALIYOFANYIWA UCHUNGUZI WA KINA TOKA KILA PEMBE CONTACTS: +255 787 377 722 Email: drweyunga@gmail.com PIA UNAWEZA KUNI FOLLOW KUPITIA INSTAGRAM YANGU @drweyunga | TANGAZA NASI ILI UWAFIKIE WATU WENGI ZAIDI.

Jumamosi, 31 Januari 2015

EBOLA KUENDELEA KUCHELEWESHA KUFUNGULIWA SHULE NCHINI LIBERIA

Nchi ya Liberia imechelewesha mpango wake ya kufungua shule, kutokana na madai kuwa haijajiandaa kikamilifu kuzuia kusambaa kwa ugonjwa hatari wa Ebola.

Shule zilifungwa tangu Julai mwaka jana, zilipaswa kufunguliwa siku ya jumatatu, hata hivyo sasa masomo yataanza ifikapo Februari 16.

Shule kadhaa Liberia bado hazijajiandaa kudhibiti Ebola, nyingi zikiwa hazina maji yenye klorini kwa ajili ya wanafunzi kuosha mikono yao, pamoja na kipima joto cha kubaini iwapo mwanafunzi anahoma.

Hakuna maoni :

Chapisha Maoni