Kiwanda kimoja nchini Uingereza
kimeshutumiwa kumuita sonara kukata pete za ndoa za wafanyakazi wake,
kwa madai kuwa ni taratibu za afya na usalama.
Chama cha wafanyakazi kimesema
kitendo hicho kiliwaliza wafanyakazi wa kiwanda hicho waliovuliwa
pete zao, wengine hii ikiwa ni mara ya kwanza kuvua pete zao tangu
wafunge ndoa na wenza wao.
Kiwanda hicho cha Becton Dickinson
kilichoajiri wafanyakazi wapatao 700, kimesema kilimuita sonara ili
kurekebisha pete zao ili ziweze kuvuka wakiwa kazini, baada
mfanyakazi mmoja kukatika kidole baada ya pete yake kunasa kwenye
mashine.
Hakuna maoni :
Chapisha Maoni