Mtaalam wa silaha za kemikali wa
kundi hatari la Dola ya Kiislam (IS) nchini Irak ameuwawa katika
mashambulizi ya anga yanayoendeshwa na Marekani na washirika wake.
Marekani imesema mtaalam huyo Abu
Malik alikuwa akitoa mafunzo kwa IS, ya kuwawezesha kufanikisha kuwa
na uwezo wa kutengeneza silaha za kemikali.
Malik alikuwa ni mhandisi wa silaha
za kemikali katika utawala wa rais Saddam Hussein, kabla ya kujiunga
na al-Qaeda nchini Irak na baadae kujiunga na IS.
Marekani na washirika wake wamefanya
mashambulizi ya anga yapatao 2,000 yanalolilenga kundi la IS.
Hakuna maoni :
Chapisha Maoni