Shirika la Ujasusi la Marekani (FBI)
limewakamata raia watatu wa kigeni ambao wakala wao wamesema walikuwa
wakijaribu kujiunga na kundi la Dola ya Kiislam (IS).
Wawili miongoni mwao ambao ni
wanaume walitishia kuwauwa maafisa polisi na mawakala wa FBI nchini
Marekani iwapo watazuiwa kwenda nchini Syria.
Wanaume hao walibainika na mamlaka
ya Marekani, baada ya kuposti vitisho hivyo kwenye tovuti ya lugha ya
Uzbek, katika miezi ya hivi karibuni. Katika moja ya posti zao
walitishia kumuua Rais Barack Obama.
Hakuna maoni :
Chapisha Maoni