.

.

.

.

.

.

.

.
KARIBUNI TUHABARIKE, TUELIMISHANE, TUPEANE HABARI ZA KUKUFANYA UTABASAMU KIDOGO NA MATUKIO YALIYOFANYIWA UCHUNGUZI WA KINA TOKA KILA PEMBE CONTACTS: +255 787 377 722 Email: drweyunga@gmail.com PIA UNAWEZA KUNI FOLLOW KUPITIA INSTAGRAM YANGU @drweyunga | TANGAZA NASI ILI UWAFIKIE WATU WENGI ZAIDI.

Alhamisi, 26 Februari 2015

KAHAWA INAYOCHANGANYWA NA SIAGI PAMOJA NA MAFUTA YA NAZI YAWA DILI


Iwapo utapatiwa kikombe cha kahawa iliyochanganywa na kijiko kimoja cha chai chenye siagi na mafuta ya nazi, huenda mtu ukapatwa na mshtuko wa moyo kutokana na mchanganyiko huo.

Lakini baada ya watafiti kubaini kuwa mafuta ni mazuri kwa binadamu kuliko sukari, na mchanganyiko huo unasaidia kupunguza mafuta mwilini, sasa kahawa hiyo imejipatia umaarufu nchini Marekani na Uingereza.

Wapenzi wa mchanganyiko huo wa kahawa na siagi, wamedai kuwa huwafanya wajihisi wamepata kifungua kinywa kilichokamilika na hupata nguvu, uongeza umakini, hupunguza kalori mwilini na kuondoa mafuta ya ziada mwilini na kujisikia shibe hadi mchana.
                     Kisu chenye siagi ambayo huchanganywa katika kikombe cha kahawa

Hakuna maoni :

Chapisha Maoni