Arsenal imekuwa na usiku mbaya, baada ya kukubali kichapo cha mabao 3-1 toka kwa wageni wao Monaco waliosafiri kutoka nchini Ufaransa, katika mchezo wa ligi ya mabingwa barani Ulaya uliochezwa usiku wa kuamkia leo.
Wakicheza mbele ya mashabiki wao waliokuwa wamefurika katika uwanja wa Emirates, Arsenal walijikuta wakikubali nyavu zao kutikiswa mara tatu kupitia kwa mabao yaliyofungwa na Geoffrey Kondogbia dakika ya 38, bao la pili la Monaco likifungwa na Dimitar Berbatov dakika ya 53.
Bao la tatau likifungwa na Ferreira Carrasco (90+4). Bao pekee la kufutia machozi la Arsenal lilifungwa na Alex Oxlade Chamberlain dakika ya 91.
Kocha mkuu wa Arseanl, Arsene Wenger ( katikati ) na benchi lake la ufundi wakiwa hawaamini kinachotokea mbele yao.
Mashabiki wa Monaco waliosafiri kutoka Ufaransa kwenda London kuishangilia timu yao dhidi ya Arsenal
Jisajili kwenye:
Chapisha Maoni
(
Atom
)
Hakuna maoni :
Chapisha Maoni